TAREHE 4/02/2017 PROF ANNA TIBAIJUKA ALITEMBELEA KIWANDA CHA MAGODORO ASILI DODOMA.
Mhe Profesa Anna Tibaijuka alitembelea kiwanda tajwa na kununua magodoro 80 kwa ajili ya kituo cha watoto walemavu wa akili cha Muyuji Chesire Home cha Dodoma. Kituo hicho kibahudumia watoto kutoka Tanzania nzima.
Gharama ya magodoro ya 80 ya 3×6 =Shs 5,672,000/- imelipwa kutokana na michango iliyofanywa na Wabunge kusaidia kituo hicho chini ya uhamasishaji na uratibu wa Profesa Anna.
Aliongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya kituo hicho Nd. Peter Mavunde ambaye anaonekana pichani na suti nyeusi.
Ilikuwa furaha kwa wanawake waajiriwa katika kiwanda hicho kumuona Profesa na kupiga picha nao. Kiwanda kinamilikiwa na HMH GULAMALI GROUP. Kinaajili watu 90.
Taarifa ya Aidan Mapala
Posted by Noel Mubeya
on Feb 8 2017. Filed under Prof Tibaijuka's Daily Photo News.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0.
Both comments and pings are currently closed.