Prof  Anna Kajumulo Tibaijuka

Tarehe 21/11/2016 Prof.Tibaijuka ameshiriki mkutano wa Wiki ya Maji Kenya uliofanyika katika ukumbi wa Kenyatta International Conference Centre(K.I.C.C)

Tarehe 21/11/2016 Prof.Tibaijuka ameshiriki mkutano wa Wiki ya Maji Kenya. Mkutano umefanyika katika ukumbi wa KENYATTA  INTERNATIONAL CONFERENCE CENTRE  (K.I.C.C) na kushirikisha wadau na taasisi mbalimbali duniani. Miongoni mwa washiriki ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji Kenya Mhe.Eugene Wamalwa, naibu Waziri mkuu na Waziri wa mambo ya nje wa Ubelgiji Mhe. Didier Reynders. Pamoja na viongozi wakuu wa nchi ya Kenya, wakuu wa taasisi mbalimbali na mabalozi. Prof. Tibaijuka anamwakilisha Dr . Chris Williams ambaye ndie mkurugenzi wa shirika la WSSCC.Katika mkutano huo Prof.Tibaijuka anahimiza sana umuhimu wa Maji, kutunza vyanzo vya Maji na mazingira. Anahimiza pia umuhimu wa usafi kwani mambo haya yanaenda kwa pamoja. Katika mkutano huo prof. Tibaijuka alikuwa kivutio kwa mada zake moto moto na ujumbe wake. Amehimiza serikali zote kutasahau wala kuacha nyuma suala la usafi. Jambo hili lilipelekea Waziri wa Maji kubadili Jina la mkutano na kukubali pendekezo la prof.Tibaijuka kwamba kuanzia mwakani mkutano hautaitwa tena Kenya Water Week, badala yake utaitwa Kenya Water Week and Sanitation ili kutosahau kuhimiza juu ya usafi kama alivyo pendekeza prof.Tibaijuka

8572f38e-19b4-46cd-84c7-43e2d9cfd90b

2321098b-ed4f-491f-aa3e-311bfeaf2f88

b1eafa6f-ac55-4adf-a813-ed17e59bca84

b4c3e87d-1184-4b4c-a62e-325acbcfae97

b255161b-06ee-4940-a69a-b6031597ac9d

be38a7aa-6261-4901-bfa7-8b4a87cde2d7

cc8f3221-6569-46c2-b908-e7c8f6a9fd65

ffe5f4f2-3a33-4392-a0d1-dd35fd949c49

Posted by on Nov 29 2016. Filed under Prof Tibaijuka's Daily Photo News. You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Both comments and pings are currently closed.

Comments are closed

Photo Gallery

Log in | This website is Designed & Maintained by Noel Mubeya