Prof  Anna Kajumulo Tibaijuka

10-02-2016 Mapokezi ya ambulance hospitali ya wilaya Rubya Jimbo la Muleba Kusini kama utekelezaji wa ahadi husika

WhatsApp Image 2017-02-10 at 17.56.05Hatimaye yaliyotabiriwa sasa yametimia. Mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 19. 09.2016 Wakati wa Ziara ya Mh. Waziri Ummy Mwlm. Muleba kule Rubya Hospital.

Mh. Mbunge Prof. Tibaijuka alimuomba Mh. Waziri kuwa baada ya Kaigara na Kimeya kupata Ambulance, ni vema tukapata Ambulance nyingine hapa Hospitali teule ya Rubya.

Mh. Waziri alikubali na leo hatimaye ahadi imetimia. Leo hii Uongozi wa Rubya umepokea rasmi Ambulance husika kama utekelezaji wa ahadi husika

Tunachukua nafasi hii kuwapongeza Wana Muleba kwa kupata Ambulance husika. Shukran zimwendee mtoa maombi na mfuatiliaji Mh. Prof. Tibaijuka a.k.a Akalandalugo kuhakikisha sasa Muleba tutakuwa na Ambulance 4, kwa maana kwamba Rubya, Kimeya na Kaigara. Ile nyingine ipo Kishuro kwa Mh. Mwijage Jimbo la Muleba Kaskazini.

Naambatanisha picha za makabidhiano.

WhatsApp Image 2017-02-10 at 17.56.02 WhatsApp Image 2017-02-10 at 17.56.03

Posted by on Feb 11 2017. Filed under Prof Tibaijuka's Daily Photo News. You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Both comments and pings are currently closed.

Comments are closed

Photo Gallery

Log in | This website is Designed & Maintained by Noel Mubeya